UK-based data, voice and IP provider for Africa, Liquid Telecom, is set to expand in Tanzania through the acquisition of Raha, the country’s leading internet service provider.
Liquid Telecom recently announced that it has received the final regulatory approval to become the majority stakeholder of Raha.
The Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) approved the agreement on December 8th, 2016.
Following the acquisition, Tanzania will become the latest market to be added to Liquid Telecom’s extensive fibre network, which is the largest of its kind serving eastern, central and southern Africa, spanning over 40,000km across 12 countries.
“We are very pleased to announce that this transaction has received its final approval. The agreement enables Liquid Telecom to expand its footprint into Tanzania, a growing and dynamic African country,” said Nic Rudnick, CEO of Liquid Telecom.
“We are thrilled with this approval and look forward to being part of a pan-African connectivity movement,” said Aashiq Shariff, CEO of Raha.
Raha today serves over 1500 businesses as well as a growing number of retail customers with a range of connectivity solutions, including fibre, satellite, WiMAX and Wi-Fi.
Liquid Telecom has operating companies in the UK and across Africa in Botswana, the DRC, Kenya, Lesotho, Rwanda, South Africa, Uganda and Zambia, and Zimbabwe.
Liquid Telecom is currently working on a new submarine cable set to run along the East African coast and into the Red Sea.
The new fibre-optic cable will help boost internet speed and mobile communication in Tanzania.
Tanzania Internet
Internet services’ users in Tanzania reached 17.3m in 2015 (34% of total population), compared to only 5.3m (12% of total population) in 2011.
The number of mobile wireless users also increased significantly during 2011–2015, from 3.7m to 16.2m, accounting for more than 90% of the total number of internet users.
The most common broadband service in Tanzania is given through 2G connections, which offers a speed of up to 0.3 Mbps and is used by 85% of the mobile subscribers in Tanzania.
Currently (2016), 3G and 4G services with speeds of up to 8Mbps are being used by 2.53m mobile subscribers across the country.
Source: tanzaniainvest
Emmanuel Mahundi
Friday, 23 December 2016
Monday, 16 February 2015
HII NDIO NJIA RAHISI AMBAYO UNAWEZA KUITUMIA KUZALISHA KUKU CHOTARA
Leo tutaangalia kuhusu ufugaji wa kuku wa kienyeji kwa
kutumia njia rahisi. Na jinsi gani unaweza kuzalisha kuku chotara. Kuku chotara
ni mchanganyiko wa kuku wa kienyeji na kisasa. Kabla hatujangalia hatua muhimu
za kuzalisha kuku chotara, tutaangalia faida za kuku chotara kwa
mwekezaji/mjasiriamali.
Faida za kuku chotara
kwa mfugaji na mlaji
Ukuaji mzuri
Nyama yake ina ladha nzuri na laini
Nyama yake ina ladha nzuri na laini
n.k
HATUA
MUHIMU KATIKA UZALISHAJI WA KUKU CHOTARA
Hatua
ya kwanza, andaa banda lako ambalo linafaa kwa matumizi ya ufugaji wa kuku,
banda la kuku linatakiwa liwe lina
pitisha hewa ya kutosha na kama unataka kufahamu kwa undani kuhusu maandalizi muhimu
ya banda lako. Makala hiyo itakuja kupitia blog yako ya uwekezaji na mtanzania.
Hatua
ya pil,i andaa kuku wa kienyeji matetea (majike) na jogoo la kisasa aina ya
kocks au aina yoyote ile ambayo inafaa, wachanganye kuku wa kienyeji na
jogoo la kisasa katika banda moja ili uweze kupata mayayi yenye mchanganyiko wa
kuku wa kienyeji na kisasa. Kumbuka jogoo mmoja (1)anatakiwa kuwa na matetea
kumi na tano (15) au matetea yasizidi kumi na tano.
Hatua
ya tatu kutotolesha mayayi ambayo umeyapata kutokana na mchanganyiko wako,
unaweza kutumia mashine za kutotolesha mayayi au unaweza kuwatumia matetea yako
ya kuku wa kienyeji kuatamia mayayi yako.
Hatua ya nne baada ya siku ishirini na moja (21), vifaranga vyako vitakuwa tayari
kwa kutumia matetea ya kuku wa kienyeji au mashine ya kutotolesha vifaranga kwa
ajilia ya matunzo mpaka wakiwa wakubwa. Vifaranga vikishakuwa tayari chanjo
muhimu wanahitaji ili kuzuia vifo na mripuko wa magonjwa. Vifaranga kwa muda wa
wiki tatu hadi nne wanahitaji joto la kutosha, kwa ajili ya ukuaji afya njema.
Chanjo
na dawa muhimu kwa vifaranga mpaka wakiwa wakubwa
Siku 2-6 Pullorum
Trisulmycine,Trimazine 30%au Cotrim+Vitalyte,Amin’total au Broiler booster maji
Siku ya 7 Mdondo(newcastle) Newcastle vaccine(Lasota maji
Siku 14 Gumboro Gumboro (Bursine vaccine-IBD) maji
Siku 16-20 Coccidiosis Trisulmycine/Trimazine/Esb3 30%+Dawa yoyote ya Vitamin maji
Siku 21 mdondo(newcastle) Newcastle vaccine(Lasota) maji
Siku 28 Gumboro Gumboro (Bursine vaccine-IBD) maji
Wiki ya 6-8 Ndui Fowl pox vaccine sindano kwenye bawa
Wiki ya 13 minyoo Pipperazine cirtrate+Dawa yoyote ya vitamin maji
Wiki ya 10 hadi ya 15 ukataji midomo Dawa ya vitamin itumike baada ya zoezi maji
Siku ya 7 Mdondo(newcastle) Newcastle vaccine(Lasota maji
Siku 14 Gumboro Gumboro (Bursine vaccine-IBD) maji
Siku 16-20 Coccidiosis Trisulmycine/Trimazine/Esb3 30%+Dawa yoyote ya Vitamin maji
Siku 21 mdondo(newcastle) Newcastle vaccine(Lasota) maji
Siku 28 Gumboro Gumboro (Bursine vaccine-IBD) maji
Wiki ya 6-8 Ndui Fowl pox vaccine sindano kwenye bawa
Wiki ya 13 minyoo Pipperazine cirtrate+Dawa yoyote ya vitamin maji
Wiki ya 10 hadi ya 15 ukataji midomo Dawa ya vitamin itumike baada ya zoezi maji
KUMBUKA
Dawa
ya minyoo na chanjo ya kideli kila baada ya miezi mitatuImeandikwa: Emmanuel Mahundi
Kutoka wekezamtanzania.blogspot.com
Wednesday, 28 January 2015
HAYA NI KATI MAGONJWA AMBAYO HUWASUMBUA KUKU
1. Mafua ya kuku (Fowl
coryza)
Mafua kwa kuku mara nyingi husababisha na bacteria, ila mara zote chanzo
kikubwa cha ugonjwa huu ni kutokuwa na usafi mzuri wa banda la kuku.
Dalili za ugonjwa
huu: kuku kuhema kwa shida, kukoroma, kutiririsha kamasi puani, utelezi wa
kamasi mdomoni na kuku kuvaa koti. Ili kuweza kutambua dalili za ugonjwa mapema
ni vizuri ukiwa unawapa chakula kuku kuwaangalia kwa a makini.
Matibabu: Usafi wa banda, kuwatenga kuku ambao wanahumwa, kuchanja
kuku na kuwapa antibiotic kama OTC 20%, OTC 50%, sulphamethazine, streptomycine na vitamin. Dawa nyingine
vitunguu swaumu robo vimenye, twanga, changanya maji lita moja, chuja na uwape
kuku kwa wiki moja vile vile husaidia kutibu homa ya matumbo
2. Ndui ya
kuku (Fowl pox)
Kuku hupatwa na malenge kwenye kishungi na sehemu
zisizo na manyoya, vile vile kuku kuvimba macho na kuwa na usaha.
Matibabu: kuku wachanje wakiwa na umri
wa miezi miwili na wale ambao wameambukizwa watengwe na kupatiwa salfa.
Mara nyingi ugonjwa huu unasababishwa na vyombo
kutokuwa safi na kuku kupata choo cheupe.
Dalili za
ugonjwa:
kuku kuharisha nyeupe, kuku kupoteza hamu ya kula, kuku kusinzia, na kuku kuvaa
makoti.
Matibabu: usafi wa vyombo,
usafi wa banda, watenge kuku wagonjwa na kuwapatia dawa Amporium, Typhoprim Furazolidone
au Sulfadimidine.
Kwa maelezo zaidi/ushauri tuma ujumbe mfupi kwa
emmanuelmahundi@gmail.com
Thursday, 22 January 2015
Mambo ya msingi kuyafahamu kabla ujaanza ufugaji wa kuku
Biashara ya ufugaji inahitaji maandali kama zilivo
biashara zingine. Ufugaji wa kuku unahitaji maandali ya msingi ili uweze
kufanya kwa ufanisi na ubora. Maandalizi yanamuhusu mfugaji kujifunza vitu
vingi ambavyo vinahusiana na ufugaji wa kuku.
Hivi ni vitu vya msingi kuvifahamu kabla ujaingia
katika ufugaji
Jifunze
kuhusu ufugaji wa kuku
Katika kujifunza huku, tafuta watu ambao
wanajishughulisha na ufugaji wa kuku kulinga na aina ya kuku ambao unahitaji
kufuga au kupitia semina na mtandao kama huu. Katika kujifunza zingatia vitu
vya msingi kama vile aina ya kuku, ukubwa wa banda, magonjwa na soko la kuku.
Ukubwa
wa banda pamoja na idadi ya kuku
Kama mjasiriamali ambaye umehamua kuingia katika
biashara ni vizuri ukatafuta watu wazoefu au wataalamu kujua ni aina gani ya
banda linafaa katika mazingira yako. Vile vile kufahamu ukubwa wa banda na
idadi ya kuku, ili usije ukajenga banda ambalo haliendani na idadi ya kuku na
kusababisha kuku kukua kwa shida na kuambukizana magonjwa.
Aina
ya kuku
Vile vile kama mfugaji anatakiwa kuwa makini katika
kuchagua aina bora ya kuku wa kufuga. Aina ya kuku ina mchango mkubwa katika
biashara hii. Kuku wengine hushambuliwa sana na magonjwa, hawatagi vizuri au
ukuajia wake ni wa taratibu. Kwa kama mfugaji lazima uwe na taarifa ya aina ya
kuku ambao ni bora.
Kuhusu
chakula cha kuku
Ili kuku wakue vizuri wanahitaji mchanganyiko ya
chakula ambacho kinakizi mahitaji yao. Kwa hiyo ni vema kwa mfugaji kuwa na fomula
ya uchanganyaji wa chakula au kununua chakula ambacho ni bora. Kwa sababu
ukuajia wa kuku unategemea asilimia kubwa kutoka katika chakula wanachokula.
Usafi
wa banda
Sehemu kubwa ya magonjwa ya kuku yanatokana na banda
kutokuwa usafi ukiachilia magonjwa ya milipuko. Kwa ni vizuri kuhakikisha kuwa
banda la kuku linakuwa safi pamoja na vyombo vya chakula pamoja na maji. Vitu
hivi visipokuwa safi mara nyingi huchangia kuku kupata magonjwa.
Magonjwa
yanayowasumbua kuku
Mfugaji ni vizuri ukawa na taarifa na kujifunza
kuhusu magonjwa ambayo huwashambulia kuku. Ni vizuri ukajifunza dalili zake na
tiba ya magonjwa mbalimbali na jinsi ya kuyazuia. Vile vile ukajifunza katika
kuwapa kuku chanjo zao katika muda muafaka.
Ukajifunza
jinsi kupata masoko
Kama mjasiriamali ni vizuri ukajifunza mapema kuhusu
jinsi ya kupata masoko ya bidhaa zako kama vile mayai na kuku. Upatikana wa
soko ndio kitu kitakochafanya biashara yako izidi kustawi na kukua. Unatakiwa
kufahamu soko la bidhaa yako mapema ili kuwa na uhakika na biashara yako.
Haya yote
utajifunza wapi?
Sehemu kubwa ya kupata maarifa haya tembelea mtandao
huu kila siku na upate kujifunza mambo mengi kuhusu ufugaji wa kuku.
Wednesday, 21 January 2015
Haya ndio magonjwa ambayo kuku huyapata
Ufugaji wa kuku kuna changamoto kubwa ya kuku kupata
magonjwa ambayo yataathiri ukuaji wake au kuku kufa. Magonjwa mengi kuku
huyapata kutokana na banda kutokuwa safi, kuingia kwa ugonjwa katika banda,
kutofuata taratibua za kinga na magonjwa ya mlipuko.
Haya ni kati magonjwa
ambayo kuku huyapata katika vipindi tofauti vya ukuaji wake
Kuharisha damu
Dalili ya kuku kuharisha damu kama vile kuku kupata kinyesi
cha damu, kuku kushuka mabawa na kuku kutochangamka.
Kutibu; usafi wa
banda la kuku, kuwatenga kuku wenye homa na vile vile tumia dawa ya amporium,
Typhoprim, Esb3 n.k
Kideri (Newcastle)
Husababishwa
na virusi na dalili zake kama kuku kupumua kwa shida, kuku kuhara na kuku hufa
wengi kwa mkupuo.
Kutibu; kuku wachanjwe katika
juma la kwanza, baada ya wiki mbili, baada ya kufikisha miezi mine na kila
baada ya miezi miwili au mitatu.
Endelea
kutembelea mtandao huu kujifunza magonjwa zaidi ambayo kuku huyapata.
Nakutakia mafanikioa mema katika maisha yako mwaka 2015
Kwa maelezo zaidi/ushauri tuma ujumbe mfupi kwa
Subscribe to:
Posts (Atom)