Wednesday, 21 January 2015

Haya ndio magonjwa ambayo kuku huyapata



Ufugaji wa kuku kuna changamoto kubwa ya kuku kupata magonjwa ambayo yataathiri ukuaji wake au kuku kufa. Magonjwa mengi kuku huyapata kutokana na banda kutokuwa safi, kuingia kwa ugonjwa katika banda, kutofuata taratibua za kinga na magonjwa ya mlipuko.













Haya ni kati magonjwa ambayo kuku huyapata katika vipindi tofauti vya ukuaji wake

Kuharisha damu
Dalili ya kuku kuharisha damu kama vile kuku kupata kinyesi cha damu, kuku kushuka mabawa na kuku kutochangamka.
Kutibu; usafi wa banda la kuku, kuwatenga kuku wenye homa na vile vile tumia dawa ya amporium, Typhoprim, Esb3 n.k

Kideri (Newcastle)
Husababishwa na virusi na dalili zake kama kuku kupumua kwa shida, kuku kuhara na kuku hufa wengi kwa mkupuo.
Kutibu; kuku wachanjwe katika juma la kwanza, baada ya wiki mbili, baada ya kufikisha miezi mine na kila baada ya miezi miwili au mitatu.

Endelea kutembelea mtandao huu kujifunza magonjwa zaidi ambayo kuku huyapata.

Nakutakia mafanikioa mema katika maisha yako mwaka 2015

Kwa maelezo zaidi/ushauri tuma ujumbe mfupi kwa

No comments:

Post a Comment