Wednesday, 28 January 2015

HAYA NI KATI MAGONJWA AMBAYO HUWASUMBUA KUKU



1. Mafua ya kuku (Fowl coryza)
Mafua kwa kuku mara nyingi husababisha na bacteria, ila mara zote chanzo kikubwa cha ugonjwa huu ni kutokuwa na usafi mzuri wa banda la kuku.












Dalili za ugonjwa huu: kuku kuhema kwa shida, kukoroma, kutiririsha kamasi puani, utelezi wa kamasi mdomoni na kuku kuvaa koti. Ili kuweza kutambua dalili za ugonjwa mapema ni vizuri ukiwa unawapa chakula kuku kuwaangalia kwa a makini.

Matibabu: Usafi wa banda, kuwatenga kuku ambao wanahumwa, kuchanja kuku na kuwapa antibiotic kama OTC 20%, OTC 50%, sulphamethazine, streptomycine na vitamin. Dawa nyingine vitunguu swaumu robo vimenye, twanga, changanya maji lita moja, chuja na uwape kuku kwa wiki moja vile vile husaidia kutibu homa ya matumbo

2. Ndui ya kuku (Fowl pox)
Kuku hupatwa na malenge kwenye kishungi na sehemu zisizo na manyoya, vile vile kuku kuvimba macho na kuwa na usaha.







Matibabu: kuku wachanje wakiwa na umri wa miezi miwili na wale ambao wameambukizwa watengwe na kupatiwa salfa.

3. Kuharisha nyeupe (homa ya matumbo)
Mara nyingi ugonjwa huu unasababishwa na vyombo kutokuwa safi na kuku kupata choo cheupe.

Dalili za ugonjwa: kuku kuharisha nyeupe, kuku kupoteza hamu ya kula, kuku kusinzia, na kuku kuvaa makoti.

Matibabu: usafi wa vyombo, usafi wa banda, watenge kuku wagonjwa na kuwapatia dawa Amporium, Typhoprim Furazolidone au Sulfadimidine.

Kwa maelezo zaidi/ushauri tuma ujumbe mfupi kwa
emmanuelmahundi@gmail.com

No comments:

Post a Comment