Thursday, 22 January 2015

Mambo ya msingi kuyafahamu kabla ujaanza ufugaji wa kuku



Biashara ya ufugaji inahitaji maandali kama zilivo biashara zingine. Ufugaji wa kuku unahitaji maandali ya msingi ili uweze kufanya kwa ufanisi na ubora. Maandalizi yanamuhusu mfugaji kujifunza vitu vingi ambavyo vinahusiana na ufugaji wa kuku.












Hivi ni vitu vya msingi kuvifahamu kabla ujaingia katika ufugaji

Jifunze kuhusu ufugaji wa kuku
Katika kujifunza huku, tafuta watu ambao wanajishughulisha na ufugaji wa kuku kulinga na aina ya kuku ambao unahitaji kufuga au kupitia semina na mtandao kama huu. Katika kujifunza zingatia vitu vya msingi kama vile aina ya kuku, ukubwa wa banda, magonjwa na soko la kuku.

Ukubwa wa banda pamoja na idadi ya kuku
Kama mjasiriamali ambaye umehamua kuingia katika biashara ni vizuri ukatafuta watu wazoefu au wataalamu kujua ni aina gani ya banda linafaa katika mazingira yako. Vile vile kufahamu ukubwa wa banda na idadi ya kuku, ili usije ukajenga banda ambalo haliendani na idadi ya kuku na kusababisha kuku kukua kwa shida na kuambukizana magonjwa.

Aina ya kuku
Vile vile kama mfugaji anatakiwa kuwa makini katika kuchagua aina bora ya kuku wa kufuga. Aina ya kuku ina mchango mkubwa katika biashara hii. Kuku wengine hushambuliwa sana na magonjwa, hawatagi vizuri au ukuajia wake ni wa taratibu. Kwa kama mfugaji lazima uwe na taarifa ya aina ya kuku ambao ni bora.

Kuhusu chakula cha kuku
Ili kuku wakue vizuri wanahitaji mchanganyiko ya chakula ambacho kinakizi mahitaji yao. Kwa hiyo ni vema kwa mfugaji kuwa na fomula ya uchanganyaji wa chakula au kununua chakula ambacho ni bora. Kwa sababu ukuajia wa kuku unategemea asilimia kubwa kutoka katika chakula wanachokula.

Usafi wa banda
Sehemu kubwa ya magonjwa ya kuku yanatokana na banda kutokuwa usafi ukiachilia magonjwa ya milipuko. Kwa ni vizuri kuhakikisha kuwa banda la kuku linakuwa safi pamoja na vyombo vya chakula pamoja na maji. Vitu hivi visipokuwa safi mara nyingi huchangia kuku kupata magonjwa.

Magonjwa yanayowasumbua kuku
Mfugaji ni vizuri ukawa na taarifa na kujifunza kuhusu magonjwa ambayo huwashambulia kuku. Ni vizuri ukajifunza dalili zake na tiba ya magonjwa mbalimbali na jinsi ya kuyazuia. Vile vile ukajifunza katika kuwapa kuku chanjo zao katika muda muafaka.

Ukajifunza jinsi kupata masoko
Kama mjasiriamali ni vizuri ukajifunza mapema kuhusu jinsi ya kupata masoko ya bidhaa zako kama vile mayai na kuku. Upatikana wa soko ndio kitu kitakochafanya biashara yako izidi kustawi na kukua. Unatakiwa kufahamu soko la bidhaa yako mapema ili kuwa na uhakika na biashara yako.

Haya yote utajifunza wapi?
Sehemu kubwa ya kupata maarifa haya tembelea mtandao huu kila siku na upate kujifunza mambo mengi kuhusu ufugaji wa kuku.



No comments:

Post a Comment