Kuku ni jamii ya ndege ambao hufuga katika mazingira kawaida ambayo
binadamu wanaishi. Kuna aina nyingi za kuku a) kuku wa kienyeji b) kuku wa kisasa.
Katika ufugaji wa kuku kuana aina tofauti za ufugaji wa kuku ambazo hutumika.
Katika somo la leo tutaangalia ufugaji wa kuku wa kienyeji katika mazingira ya
kawaida.
Katika kuchagua aina ya ufugaji wa kuku hutokana na mahitaji
husika na gharama za kutengeneza banda pamoja na chakula.
Hizi ndio njia 3
unazoweza kutumia kufuga kuku katika mazingira ya kawaida
Ufugaji wa kuku huria
Katika ufugaji huu kuku hujitafutia chakula wao wenyewe.
Ufugaji wa kuku huria unahitaji kuwa na eneo kubwa ambalo kuku wataweza
kujitafutia chakula chao wao wenyewe. Ufugaji wa kuku huria hauna gharama kubwa
za uendeshaji na kuku hulala eneo ambalo sio rasmi. Faida za ufugaji wa kuku
huria; unahitaji gharama ndogo, ni njia rahisi na kuku wanapata mazoezi ya
kutosha.
Hasara za kufuga kuku huria ni rahisi kupata magonjwa,
ukuaji wa kuku ni mdogo na kuna hatari ya kupata magonjwa.
Ufugaji wa kuku nusu huria (nusu ndani – nusu nje)
Katika ufugaji huu kuku wanakuwa wanaishi nje ambapo panauwa
pamezungushiwa uzio na kuna kuwa na banda ambalo hutumia kutagia, kuatamia na
kulala. Katika ufugaji inakuwa rahisi kuwa chakula, kudhibiti magonjwa,
utaepusha uwezekano wa kuku kuibiwa na kuweza kuwatambua kuku wagonjwa.
Changamoto ya kufuga kuku nusu huria unahitaji gharama
kubwa, unahitaji eneo kubwa na unahitaji muda mwingi kuwepo ili kuwangalia na
kuwapa chakula.
Ufugaji wa kuku ndani ya banda
Ni ufugaji ambao kuku wanaishi katika banda kwa muda wote
bila kutoka nje. Katika ufugaji kuku wanahitaji kupewa chakula bila ya wao
wenyewe kujitafutia. Katika ufugaji unahitaji kuandaa banda bora kuku. Faida ya
ufugaji wa kuku ndania ya banda kama ni rahisi kudhubiti maonjwa na upotevu wa
mayai, vile vile ni rahsi katika kuwapatia chakula kulingana na makundi ya
kuku.
Changamoto za ufugaji huu ni gharama kubwa kuandaa banda na
kuwapatia chakula, ni rahisi ugonjwa ukiingia kuambukizana kuku wote.
Nakutakia mafanikioa mema katika maisha yako mwaka 2015
Kwa maelezo zaidi/ushauri tuma ujumbe mfupi kwa
emmanuelmahundi@gmail.com
No comments:
Post a Comment